Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 34 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 444 | 2025-05-28 |
Name
Oliver Daniel Semuguruka
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kuzipatia maji Kata za Ikuza, Mazinga, Kerebe, Goziba na Bumbire zilizopo Ziwa Victoria?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza inapatikana katika maeneo yote nchini ikiwemo maeneo ya Kata za Ikuza, Mazinga, Kerebe, Goziba na Bumbire zilizopo Ziwa Victoria. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa miradi ya maji itakayonufaisha Kata hizo tano zilizopo ndani ya Ziwa Victoria.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 itakarabati Skimu za Iroba, Kinagi, Goziba na Ikuza zilizopo katika Kata hizo ili ziendelee kutoa huduma ya maji kwa wananchi kwa ufanisi wakati taratibu za kutekeleza miradi mipya zikiendelea.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved