Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 34 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 445 | 2025-05-28 |
Name
Stephen Lujwahuka Byabato
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukoba Mjini
Primary Question
MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza:-
Je, Serikali imefikia hatua gani katika jitihada zake za kuwekeza mtaji katika Kiwanda cha Kahawa cha TANICA - Bukoba Mjini?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Kiwanda cha Kahawa cha TANICA kinamilikiwa na Kagera Cooperative Union - KCU kwa 53.37%, Karagwe District Cooperative Union - KDCU kwa 31.83%, Msajili wa Hazina 7.67%, Tanzania Federation of Cooperative - TFC 6.22% na Wafanyakazi wa TANICA 0.91%.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilifanya tathmini ya kiwanda hicho na kubaini kuwa kiwanda hakikuwa na Bodi ya Wakurugenzi pamoja na Menejimenti nzuri. Serikali imesimamia kuundwa kwa Bodi ya Wakurugenzi na kwa sasa kiwanda kinaendelea kufanyia kazi ushauri mbalimbali unaotolewa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kushirikiana na wanahisa wakuu wa kiwanda ili kumtafuta mwekezaji mahiri atakayeingiza mtaji kwenye Kampuni ya TANICA. Ninakushukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved