Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 155 2026-04-21

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, lini majengo mapya ya Mahakama ya Mwanzo Nanyamba yatajengwa?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Tanzania inaendelea kutekeleza Mpango wa Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Mahakama wa mwaka 2021/2022 – 2025/2026. Kutokana na uhaba wa majengo ya Mahakama hususan majengo ya Mahakama za Mwanzo katika maeneo mbalimbali nchini, majengo haya yanajengwa na kukarabatiwa kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa, tunakamilisha kutengeneza Mpango wa Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Mahakama awamu ya tatu. Aidha, ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo Nanyamba utazingatiwa katika Mpango huo.