Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 13 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 156 | 2026-04-21 |
Name
Taska Restituta Mbogo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -
Je, kwa nini Mahindi yanayovunwa kutokana na Mbegu za kisasa hayawezi kupandwa kwa mara ya pili?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mkulima hulazimika kununua mbegu kila msimu ili aweze kupata tija iliyodhamiriwa kwa sababu mbegu anazonunua katika maduka ya pembejeo huwa zimepitia majaribio ya kisayansi katika maabara ili kuthibitisha ubora wa sifa mbalimbali ikiwemo kiwango cha uzalishaji, uhimilivu wa magonjwa na ukame. Mkulima anapovuna mazao na kutumia mbegu kwa mara ya pili au zaidi husababisha sifa stahiki za mbegu husika kupungua au kupotea.
Mheshimiwa Spika, asilimia kubwa ya mbegu zinazotumiwa na wakulima nchini ni mbegu aina ya chotara ambazo utengenezaji wake hutumia aina mbili au zaidi tofauti za mbegu wazazi kutoka jamii moja. Kutokana na sababu hiyo, iwapo mbegu hizo zitatumika kama mbegu kwa mara ya pili au zaidi husababisha kupotea au kupungua kwa ubora wa mbegu hizo na hivyo kuchangia kushuka kwa tija na uzalishaji.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved