Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 157 2026-04-21

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka Mawasiliano ya simu katika Vijiji vinne vya Kata za Nyamigogo na maeneo mengine yenye uhitaji Wilayani Biharamulo?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, ninaomba kujibu swali la Mhandisi Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote imejenga Minara 11 ya Mawasiliano katika awamu mbalimbali (Awamu ya Kwanza A, Awamu ya Pili B na Awamu ya Nne B) katika kata kadhaa zilizopo katika Wilaya ya Biharamulo, ikiwemo Biharamulo Mjini, Kalenge, Kaniha, Lusahunga, Nemba, Nyabusozi, Nyakahura, Nyarubungo na Ruziba.

Mheshimiwa Spika, aidha, kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijiti Awamu ya Kwanza Minara 13 imejengwa katika kata 13 na tayari inatoa Huduma za Simu na data kwa teknolojia za 2G, 3G na 4G. Vilevile, Serikali inaendelea na ujenzi wa Mnara mmoja katika Kata ya Lusahunga chini ya Mradi wa Mawasiliano Vijijini Awamu ya 10, unaotarajiwa kuhudumia Kijiji cha Kikoma na maeneo ya jirani.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, bado kuna changamoto ya huduma za mawasiliano katika baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Biharamulo, hususan katika Kata za Nyamigogo, Runazi, Nemba na Nyakahura.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia UCSAF imebaini uwepo wa changamoto ya Huduma za Mawasiliano katika Vijiji vya Nyamigogo, Kagoma, Kasozibakaya, Songambele na maeneo mengine katika Vijiji vya Migango, Kaluguyu na Busiri. Kwa sasa, upembuzi yakinifu unaendelea ili kuyaingiza maeneo hayo katika Mpango Mkakati wa Ujenzi wa Minara wa Mwaka 2025 – 2030.