Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Eng. Ezra John Chiwelesa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Biharamulo Magharibi
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mawasiliano ya simu katika Vijiji vinne vya Kata za Nyamigogo na maeneo mengine yenye uhitaji Wilayani Biharamulo?
Supplementary Question 1
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa nafasi. Pia, ninaishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri ambayo wameyatoa na ninashukuru kwa miradi hii ambayo imefanyika. Ni kweli minara hii imejengwa na haya maeneo yanapata mawasiliano, lakini kama Serikali ilivyojibu Kata ya Nyamigogo ina vijiji vinne na vyote hakuna hata kijiji kimoja chenye mawasiliano.
Mheshimiwa Spika, eneo hili la Migango, Kata ya Runazi, ambalo umelitaja lina wakazi zaidi ya 10,000 lakini hawana mawasiliano kabisa. Ninajua mmesema ipo kwenye mpango; mpango ni 2025 – 2030. Kwa kuwa hawa watu ni wengi na wanategemea mawasiliano, ninaweza kupata kauli thabiti ya Serikali inayonihakikishia kwamba haitaweza kusubiri mpaka mwishoni kwa sababu bajeti inafanyika kila mwaka? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nipate kauli ya Serikali inayoweza kuni-assure kwamba mpango utakapoanza, hawa wananchi watapelekewa hiyo huduma haraka ili waweze kupata sub-station kwa sababu ni wengi na wanahitaji huduma ya simu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Mheshimiwa Waziri amesema Kijiji cha Busiri feasibility study inaendelea, lakini jirani na Busiri kuna eneo moja linaitwa Iloganzara kwenye Kata ya Nyakahura. Kuna Kata ya Bisibo eneo la Rwakilinda na Muungano, ni maeneo yenye watu wengi sana lakini hawana mawasiliano pia.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninaomba kupata kauli ya Mheshimiwa Waziri na Serikali kwamba hata haya maeneo mawili yatakuwa considered kwenye kufanya feasibility study ili mtakapoanza kujenga hii minara Biharamulo, basi na wao waweze kupata mawasiliano haya kwa ajili ya kuendeleza huduma za wananchi. (Makofi)
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, ninaomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kwa pamoja kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, katika maeneo yote aliyoyataja, kwa sababu amesema kuna changamoto kubwa ya mawasiliano, tutayapa kipaumbele kikubwa katika mkakati wetu tunaoendelea kuutekeleza.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya udharura alioueleza, ninamwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa UCSAF apeleke wataalamu kule katika hali ya udharura ili wakague na kufanya tathmini katika maeneo hayo kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunaweka mawasiliano mapema ili wananchi wengi aliowataja katika maeneo hayo waweze kupata mawasiliano ya uhakika. (Makofi)
Name
Sikudhani Yasini Chikambo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mawasiliano ya simu katika Vijiji vinne vya Kata za Nyamigogo na maeneo mengine yenye uhitaji Wilayani Biharamulo?
Supplementary Question 2
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Spika, viko baadhi ya vijiji mpaka leo havina minara kama alivyosema hapo Mheshimiwa Waziri. Kipekee ninaomba nizungumzie Kijiji cha Mtengashari kilichopo Kata ya Ligunga katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru. Kijiji kile hakina mawasiliano kabisa, wananchi wale wanapata shida. Ni nini sasa mkakati wa Serikali katika kuhakikisha tunakwenda kujenga minara katika kijiji kile na wananchi wetu waendelee kupata huduma ya mawasiliano? (Makofi)
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali katika kujenga minara tumeuweka katika mkakati wetu mahsusi wa Serikali wa miaka mitano ambapo tunakusudia kuyafikia maeneo yote yenye changamoto ya mawasiliano nchini ukianza na maeneo ambayo yana changamoto kubwa. Tumeyatenga katika maeneo yenye changamoto kubwa sana, changamoto za kati na changamoto ndogo.
Mheshimiwa Spika, tutaanza na maeneo yenye changamoto kubwa katika mkakati wetu wa miaka mitano na ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafika pia katika maeneo yake kwa ajili ya kuweka mawasiliano ya uhakika kwa wananchi.
Mheshimiwa Spika, ninamhakikishia kwamba ndani ya hii miaka mitano mkakati wetu utakapokamilika kila eneo lenye changamoto ya mawasiliano hapa nchini litakuwa limepata mawasiliano ya uhakika. (Makofi)
Name
Japhael Masanja Lufungija
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ulyankulu
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mawasiliano ya simu katika Vijiji vinne vya Kata za Nyamigogo na maeneo mengine yenye uhitaji Wilayani Biharamulo?
Supplementary Question 3
MHE. JAPHAEL M. LUFUNGIJA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa nafasi. Jimbo la Ulyankulu ni miongoni mwa majimbo yenye hali ngumu ya kimawasiliano hasa katika Kata ya Uyowa, Kijiji cha Mwamnange chenye wakazi wengi na kijiji cha kibiashara Kata za Sasu, Ilege na Nhwande kwa maana ya Kata ya Mwongozo. Lini Wizara itakwenda kujenga minara kwenye maeneo hayo ili wananchi waweze kunufaika? (Makofi)
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, tunatambua changamoto ya mawasiliano iliyopo katika jimbo hili na hivi karibuni, ninadhani wiki hii iliyopita wataalamu wa UCSAF walikuwa kwenye eneo la jimbo hili kufanya tathmini. Tunasubiri taarifa yao ili utekelezaji uanze kufanyika.
Mheshimiwa Spika, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya taarifa hiyo ya wataalamu kuwasilishwa Wizarani tutafanya mpango wa dharura wa kuhakikisha kwamba katika maeneo ambayo hayana mawasiliano kabisa katika Jimbo lake la Ulyankulu yanafanyiwa kazi, ninashukuru.
Name
Rashid Mohamed Mtima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Newala Mjni
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mawasiliano ya simu katika Vijiji vinne vya Kata za Nyamigogo na maeneo mengine yenye uhitaji Wilayani Biharamulo?
Supplementary Question 4
MHE. RASHID M. MTIMA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza katika Wizara hii.
Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itatatua tatizo la upatikanaji wa simu katika maeneo yafuatayo katika Jimbo la Newala Mjini: Kata ya Nanguruwe, Kijiji cha Nanguruwe, Mnanje, na Mtawe; Kata ya Mcholi I, Kijiji cha Chikwedu na Chiunjila; Kata ya Namiyonga, Kijiji cha Nakachela na Mandumba; Kata ya Mnekachi Kijiji cha Kazamoyo; na Kata ya Mtumachi, Kijiji cha Mcholi Godauni? (Makofi)
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimekuwa nikieleza katika majibu yangu kwamba Serikali imeandaa mkakati wa miaka mitano wa kuyafikia maeneo yote nchini ambayo yana changamoto ya mawasiliano. Kwa hiyo, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge katika mkakati wetu wa miaka mitano maeneo yake hayo pia tutayafikia, lakini kwa sababu ameeleza kwamba ana changamoto kubwa, tutayapa kipaumbele wakati wa kutekeleza mkakati wetu huu wa Serikali, ninakushukuru.
Name
Ester Edwin Malleko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Mawasiliano ya simu katika Vijiji vinne vya Kata za Nyamigogo na maeneo mengine yenye uhitaji Wilayani Biharamulo?
Supplementary Question 5
MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana. Ninaomba kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Kata ya Mamba Kusini katika Jimbo la Vunjo imekuwa na changamoto kubwa sana ya mawasiliano. Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu ili tuweze kupata mawasiliano ya uhakika? (Makofi)
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, kata aliyoieleza Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo la Vunjo pia itahusishwa katika mkakati wetu wa Wizara, kwa sababu pia amesema kwamba ina changamoto kubwa. Ni kati ya zile kata ambazo na sisi tumepanga kwamba katika maeneo yenye changamoto kubwa tutayapa kipaumbele tunapoendelea na utekelezaji wa mkakati wetu huu wa Wizara.
Mheshimiwa Spika, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatoa kipaumbele kikubwa kwa Jimbo lake la Vunjo katika maeneo yote yenye changamoto kubwa, hasa wakati wa utekelezaji wa mkakati mahsusi wa Wizara wa hii miaka mitano tunayoendelea na utekelezaji wake. (Makofi)