Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 22 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 248 | 2026-05-05 |
Name
Cornel Lucas Magembe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chato Kaskazini
Primary Question
MHE. CORNEL L. MAGEMBE aliuliza: -
Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa Shule za Msingi Nyamirembe, Nyabugere, Katende na Magiri ambazo zimechakaa sana?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Cornel Lucas Magembe, Mbunge wa Jimbo la Chato Kaskazini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu chakavu au ujenzi wa miundombinu mipya katika shule ambazo miundombinu yake haiwezi kukarabatiwa. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2025/2026 Serikali imetoa shilingi bilioni 3.09 kwa ajili ya ujenzi shule za msingi 11, madarasa 153 katika shule chakavu 24 na ukamilishaji wa madarasa matatu katika Shule za Msingi Nyamirembe na Magiri Wilayani Chato.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali imetenga shilingi 150,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa sita katika Shule za Msingi Katende na Nyarubugere. Aidha, Serikali itaendelea kutenga fedha za ukarabati au ujenzi wa miundombinu mipya katika shule za msingi chakavu nchini ikiwemo Shule za Msingi Nyamirembe, Nyabugere, Katende na Magiri, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved