Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 22 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 250 | 2026-05-05 |
Name
Selina Henry Kingalame
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SELINA H. KINGALAME aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaajiri wahitimu wahadhiri wa vitendo wanaojitolea sehemu za ofisi na vyuo hasa waliojitolea kwa zaidi ya mwaka?
Name
Regina Ndege Qwaray
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Selina Henry Kingalame, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma, Toleo la 2 la mwaka 2008, ikisomwa pamoja na Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura 298, ajira katika utumishi wa umma hupatikana kwa ushindani na uwazi. Kwa kuzingatia kuwa kuna vijana wanaojitolea katika sekta ya elimu na sekta nyingine za umma, Serikali ilitoa mwongozo wa kujitolea wa mwaka 2025 ili kuwezesha vijana kujipatia ujuzi wa ziada pamoja na kuwapa uzoefu na uwezo wa kushindana pindi ajira zinapotangazwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa upatikanaji wa walimu wa vyuo yaani wahadhiri, Serikali na vyuo vikuu imeweka utaratibu maalum wa kuwabaini, kuwabakiza na kuwajengea uwezo vijana wanaohitimu na ufaulu mzuri unaokidhi vigezo vya kuajiriwa kama wanataaluma katika vyuo husika. Aidha, vijana hao wanajengewa utamaduni wa kufanya kazi katika mazingira ya kitaaluma kwa utaratibu wa mikataba, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved