Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 22 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 251 | 2026-05-05 |
Name
Japhael Masanja Lufungija
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ulyankulu
Primary Question
MHE. JAPHAEL M. LUFUNGIJA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga maghala ya kuhifadhia mazao Kata ya Uyowa katika kitovu cha biashara Mwamnange ambapo tayari eneo lipo?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Wizara imepanga kufanya tathmini ya maeneo mapya ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi na ukarabati wa ghala. Tathmini hiyo itasaidia kubaini mahitaji ya uwezo wa kuhifadhi mazao katika maeneo mbalimbali nchini na hivyo kuiwezesha Serikali kutenga bajeti ya kuanza utekelezaji wa ujenzi wa ghala.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kumhakikishia Mheshimiwa Japhael Masanja Lufungija kuwa suala lake limechukuliwa na litafanyiwa kazi na Serikali baada ya kufanya tathmini kwenye kata ya Uyowa katika center ya kibiashara Mwamnange.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved