Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 22 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 252 | 2026-05-05 |
Name
Dr. Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Primary Question
MHE. DKT. SELEMANI S. JAFO aliuliza: -
Je, lini mradi wa maji kutoka Kisarawe Mjini kwenda Kata za Kazimzumbwi, Masaki, Msimbu, Kibuta hadi Marumbo utaanza kujengwa?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Selemani Saidi Jafo, Mbunge wa Kisarawe, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa kufikisha huduma ya maji safi na salama kwenye kata tano za Kazimzumbwi, Masaki, Msimbu, Kibuta pamoja na Marumbo zilizopo Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani. Miongoni mwa kazi zinazotarajiwa kutekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa kituo cha kupokea na kusukuma maji, ujenzi wa matanki mawili yenye jumla ya ujazo wa lita 800,000 sambamba na ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 52.1.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo ambapo unatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 13. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved