Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 14 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 170 | 2026-04-22 |
Name
Yannick Ikayo Ndoinyo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Primary Question
MHE. YANNICK I. NDOINYO aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Barabara kutoka Kigongoni hadi Wasso – Ngorongoro kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Yannick Ikayo Ndoinyo, Mbunge wa Ngorongoro, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Barabara ya Kigongoni ama Mto wa Mbu – Wasso – Loliondo yenye urefu wa kilometa 211 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa Sehemu ya Wasso – Sale kilometa 49 umekamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, mkataba wa ujenzi kwa sehemu ya Wasso – Loliondo urefu wa kilometa 10 umesainiwa, ambapo taratibu za malipo ya awali kwa mkandarasi zinaendelea. Vilevile, taratibu za manunuzi ya kuwapata wakandarasi wa ujenzi sehemu za Mto wa Mbu – Selela kilometa 23 na Selela – Engaruka kilometa 27 zinaendelea. Kwa sehemu zilizobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved