Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 15 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 171 | 2026-04-23 |
Name
Mwantatu Mbarak Khamis
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
House of Representatives
Primary Question
MHE. MWANTATU M. KHAMIS aliuliza: -
Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha Shule za Sekondari zinaondokana na Upungufu wa Vifaa vya Maabara?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantatu Mbarak Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitoa fedha za ununuzi wa vifaa vya maabara kwa ajili ya ujifunzaji na ufundishaji wa masomo ya sayansi ili kuwa na wahitimu wenye umahiri unaoendana na zama za sayansi na teknolojia.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali imetumia shilingi bilioni 3.51 kununua na kusambaza kemikali na vifaa vya maabara katika shule za sekondari 231. Vilevile, Serikali hivi sasa inaendelea na mchakato wa manunuzi yenye thamani ya shilingi bilioni 13.97 kwa ajili ya vifaa vya maabara vya shule 672.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha za ununuzi wa vifaa vya maabara katika shule za sekondari ili kuboresha mazingira ya kujifunza na ufundishaji wa masomo ya Sayansi.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved