Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Water and Irrigation Wizara ya Maji 173 2026-04-23

Name

Khalid Mussa Nsekela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. KHALID M. NSEKELA aliuliza: -

Je, lini Serikali itachukua hatua za haraka za upatikanaji wa maji safi na salama katika Zahanati, Vituo vya Afya, Masoko na Mashuleni – Kyerwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Khalid Mussa Nsekela, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha inafikisha huduma ya majisafi na salama kwenye maeneo yote yanayotoa huduma za kijamii ikiwemo shule, vituo vya kutolea huduma za afya, vituo vya mabasi na masoko. Huduma hiyo imeshapatikana kwenye baadhi ya maeneo mbalimbali nchini kupitia miradi ya maji iliyopo, sambamba na ile inayoendelea kujengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwezi Machi, 2026, Serikali imefikisha huduma ya majisafi na salama kwenye shule 9,957 na vituo 4,348 vya kutolea huduma za afya kote nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Wilaya ya Kyerwa, Serikali imefikisha huduma ya majisafi na salama kwenye Shule za Msingi na Sekondari 55 na Vituo 18 vya kutolea huduma za Afya pamoja na Hospitali ya Wilaya. Serikali itaendelea kutoa kipaumbele cha kipekee kwenye maeneo yote yanayotoa huduma za kijamii ili kuhakikisha yanafikiwa na huduma ya majisafi na salama kadiri miradi ya maji inavyotekelezwa kwenye maeneo yote nchini ikiwemo Wilaya ya Kyerwa.