Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 174 2026-04-23

Name

Bakari Bakari Shingo

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. BAKARI B. SHINGO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani kukarabati kwa dharura barabara ya Nyerere katika maeneo ya Mombasa – Gongo la Mboto na maeneo ya makaburi ya Kiltex?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bakari Bakari Shingo, Mbunge wa Ukonga kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa barabara kwa sehemu ya Mombasa hadi Gongo la Mboto kupitia mradi wa mabasi yaendeayo haraka awamu ya tatu (DRT 3). Aidha, kwa barabara ya inayopita maeneo ya makaburi ya Kiltex, tayari kuna mkandarasi anaendelea kuifanyia matengenezo kwa kuchonga tuta na kuweka tabaka la changarawe ili kuwezesha barabara kupitika majira yote ya mwaka. Kazi za matengenezo zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2026.