Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 15 | Sitting 15 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 174 | 2026-04-23 |
Name
Bakari Bakari Shingo
Sex
Male
Party
ACT
Constituent
Ukonga
Primary Question
MHE. BAKARI B. SHINGO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani kukarabati kwa dharura barabara ya Nyerere katika maeneo ya Mombasa – Gongo la Mboto na maeneo ya makaburi ya Kiltex?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bakari Bakari Shingo, Mbunge wa Ukonga kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa barabara kwa sehemu ya Mombasa hadi Gongo la Mboto kupitia mradi wa mabasi yaendeayo haraka awamu ya tatu (DRT 3). Aidha, kwa barabara ya inayopita maeneo ya makaburi ya Kiltex, tayari kuna mkandarasi anaendelea kuifanyia matengenezo kwa kuchonga tuta na kuweka tabaka la changarawe ili kuwezesha barabara kupitika majira yote ya mwaka. Kazi za matengenezo zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2026.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved