Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2000-2005 Session 12 Sitting 15 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 175 2026-04-23

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara kutoka Njiapanda ya Kongwa hadi Mpwapwa Mjini kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa George Natany Malima, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kongwa – Mpwapwa yenye urefu wa kilometa 38.45 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa jumla ya kilometa 6.45 zimejengwa kwa kiwango cha lami kuanzia Mpwapwa Mjini hadi Mwanakianga. Aidha, mkataba wa ujenzi kwa sehemu iliyobaki ya kuanzia Mwanakianga – Kongwa (urefu wa kilometa 32) umesainiwa ambapo taratibu za malipo ya awali kwa Mkandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi zinaendelea.