Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Amina Ali Mzee
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AMINA ALI MZEE K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha ongezeko la vyombo vya habari mtandaoni haliathiri maadili na utamaduni wa Taifa letu?
Supplementary Question 1
MHE. AMINA ALI MZEE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Kumekuwa na ongezeko kubwa la vyombo vya habari vya mtandaoni. Je, Bodi ya Ithibati inasimamiaje kuhakiki waandishi wa habari?
 
											Name
Hamis Mohamed Mwinjuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muheza
Answer
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA, NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, Bodi ya Ithibati lengo lake la msingi litakuwa ni kuhakikisha kwamba inasimamia weledi na maadili miongoni mwa waandishi wa habari, wakiwemo waandishi wa habari wa vyombo vinavyotekeleza majukumu yake mtandaoni. Itakuwa na jukumu la kusimamia vyote hivi ili kuhakikisha kwamba waandishi wa habari wanafanya shughuli zao kwa kufuata weledi, maadili, na kuzingatia usalama wa Taifa bila kukandamiza uhuru wa habari.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved