Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Mashimba Mashauri Ndaki
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Maswa Magharibi
Primary Question
MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Mwasayi ambacho kimepelekewa vifaatiba lakini hakina majengo ya kutosha?
Supplementary Question 1
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Spika, ninaipongeza Serikali na kuishukuru kwa kupeleka fedha hizo shilingi milioni 250 na asubuhi hii nimehakikisha kupitia Mkurugenzi wangu kwamba fedha hiyo imekwishafika. Kwa vile, wananchi wa Kata ya Zanzui na Kata ya Kadoto pia wameshaanza ujenzi wa vituo viwili vya afya kwenye hizo kata; je, Serikali iko tayari kuunga mkono juhudi za wananchi hao? (Makofi)
 
											Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita siku zote imekuwa tayari kuwaunga mkono wananchi katika ujenzi wa vituo vya huduma ya afya, kama ambavyo tayari imeshapeleka shilingi milioni 250 kwenye Kituo cha Afya cha Mwasayi. Nimhakikishie, katika Kata hizo za Zanzui na hiyo nyingine ambayo ameitaja tutahakikisha pia tunaanza kutenga fedha kwenye bajeti zetu kwa ajili ya kuchangia nguvu za wananchi katika ujenzi wa vituo hivyo vya afya kwa awamu. Ahsante sana.
 
											Name
Mohamed Lujuo Monni
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chemba
Primary Question
MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Mwasayi ambacho kimepelekewa vifaatiba lakini hakina majengo ya kutosha?
Supplementary Question 2
MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Makorongo kilianza kutumika miaka 10 iliyopita kikiwa hakina majengo ya OPD na maabara. Ninataka kujua ni lini Serikali itatoa fedha ili kukamilisha ujenzi huo? Ahsante sana.
 
											Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
								NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kwamba vipo vituo vya afya ambavyo vimeanza kutoa huduma, lakini vina upungufu wa majengo muhimu kwa ajili ya huduma hizo kikiwepo kituo cha afya ambacho Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Chemba amekitaja.
Mheshimiwa Spika, ninaomba nimhakikishie Mbunge kwamba, tayari Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI tulishaainisha vituo vya afya vyenye majengo pungufu na vituo vya afya chakavu na kongwe 203 na tayari tumeanza kuandaa bajeti kwa awamu kwa ajili ya ukarabati wa vituo hivyo vya afya ili viweze kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie pia Mheshimiwa Mbunge, majengo hayo ya maabara, wodi ya wanawake, wanaume na majengo mengine yatakwenda kujengwa kwenye kituo hicho cha afya.  Ahsante.
							
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved