Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Yustina Arcadius Rahhi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. YUSTINA A. RAHHI K.n.y. MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Mbulu?
Supplementary Question 1
MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, ni kweli TRA, Mbulu walikuwa na jengo la Ofisi limechakaa na lipo condemn, hawawezi kufanya kazi huko na ndiyo maana wanapanga katika ofisi ya halmashauri sasa kwa unyeti wa kazi za TRA, ni kwa nini Serikali isiharakishe kuwajengea ofisi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, tunajua watoza ushuru wanaokusanya kodi hawapendwi sana mitaani. Kwa ajili ya utendaji mzuri wa kazi wa Maafisa TRA, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea nyumba Maafisa TRA ikianza katika Mkoa wa Manyara? Ahsante. (Makofi)
 
											Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
								NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kabla ya kujibu maswali hayo ninaomba nimpongeze na kumshukuru sana Mheshimiwa Yustina Rahhi, maana yote hii inaonekana ni shauku ya maendeleo katika wilaya yake na hasa hasa katika suala zima la ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza, ni kweli kwamba jengo lililopo kwa sasa siyo rafiki, lakini Serikali imeona umuhimu wa ujenzi wa jengo hilo na ndiyo maana nasema mwaka unaokuja huo wa fedha 2025/2026 tutakwenda kujenga jengo hilo kwa ajili ya TRA.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, tumepokea ushauri wake suala la nyumba kwa wafanyakazi wetu, tumelichukua na litaenda kufanyiwa kazi.
							
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved