Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Mwantum Dau Haji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, lini Serikali itatengeneza barabara ya Hombolo kwa kiwango cha lami ili iweze kupitika wakati wote?
Supplementary Question 1
MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwanza nimshukuru Waziri wangu kwa hoja yake nzuri aliyoitoa hapo. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Je, lini kazi ya ujenzi itaanza katika barabara hiyo?
Swali langu la pili, je, Serikali ina mpango wa kumpata mkandarasi wa kusaini na kuendelea kufanya kazi hiyo?
 
											Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
								NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kwa pamoja ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara ni kweli ni muhimu sana. Tumekadiria iishe tarehe 31, lakini tunavyoongea ni kwamba usanifu umeshakamilika na tulikuwa tunajua itakamilika mwaka huu wa fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwanza, tumeipangia katika mwaka wa fedha unaokuja barabara hii ianze kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, mwaka ujao wa fedha 2025/2026 tumeshaiingiza kwenye mpango ili barabara hii muhimu sana katika Mji wa Dodoma huu kwenda Hombolo ianze kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.
							
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved