Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Daniel Awack Tlemai
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karatu
Primary Question
MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, lini Serikali itajengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Njiapanda - Mang’ola – Matala hadi Lalago ambayo ipo kwenye Ilani ya CCM 2020/2025?
Supplementary Question 1
MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Naibu Spika, je, kwa kuwa barabara hii kwa upande wa Lalago Serikali imeweza kutoa kilometa 65, ni mpango upi Serikali wanao kwa upande wa Karatu kwenda Mang’ola kuwasaidia wakulima na wafanyabiashara wanaopeleka mazao yao nje ya nchi kwa njia hii ya kupitia Karatu - Mang’ola?
 
											Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hii barabara ni moja, lakini tumeanza upande wa Nkoma kwenda Lalago. Kwa kuwa tumeshafanya usanifu na tumeshaitengea hata fedha katika mwaka ujao wa fedha 2025/2026, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango upo wa kuijenga hiyo barabara kuanzia Karatu kuelekea Matala. Ahsante.
 
											Name
Cecilia Daniel Paresso
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, lini Serikali itajengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Njiapanda - Mang’ola – Matala hadi Lalago ambayo ipo kwenye Ilani ya CCM 2020/2025?
Supplementary Question 2
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Katika barabara iliyotajwa, ndiyo barabara ambayo ikianzia pale Njia Panda kuna Hospitali ya Wilaya takribani kilometa tatu. Kwa umuhimu wa huduma hiyo ya afya katika eneo hilo, Serikali haioni kuna haja sasa angalau hizo kilometa chache zijengwe kwa kiwango cha lami?
 
											Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue ombi la Mheshimiwa Mbunge wa hizo kilometa tatu na Wizara tuweze kuona umuhimu wa kuijenga hiyo barabara kilometa tatu kwa ajili ya kutoa huduma katika hiyo hospitali. Ahsante.
 
											Name
Benaya Liuka Kapinga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbinga Vijijini
Primary Question
MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, lini Serikali itajengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Njiapanda - Mang’ola – Matala hadi Lalago ambayo ipo kwenye Ilani ya CCM 2020/2025?
Supplementary Question 3
MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini mwendelezo wa barabara ya Amani Makolo, Ruanda hadi Lituhi utaendelea?
 
											Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, tulishaanza kujenga hiyo barabara na kipande cha Ruanda kwenda Ndumbi. Mkandarasi amesaini, lakini ambacho tunasubiri sasa hivi mkandarasi aweze kulipwa advance ili aweze kuanza kazi site.
 
											Name
Boniphace Mwita Getere
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bunda
Primary Question
MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, lini Serikali itajengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Njiapanda - Mang’ola – Matala hadi Lalago ambayo ipo kwenye Ilani ya CCM 2020/2025?
Supplementary Question 4
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Sanzati - Nata imekuwa kero kwa muda mrefu sana na Wizara inafahamu kinachoendelea. Ni nini sasa mkakati wa Serikali wa kumaliza barabara hiyo? Nakushukuru.
 
											Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
								NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali kwa barabara zote, hasa zile ambazo wakandarasi wameshaanza, ni kuhakikisha kwamba tunazikamilisha. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mkandarasi alikuwa anasuasua kwa sababu alikuwa bado hati za malipo alizoomba zilikuwa bado hazijalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara ya Fedha imeahidi itatoa fedha muda siyo mrefu ili wakandarasi sasa waweze kuendelea na kazi ikiwa ni pamoja na hiyo barabara ya Sanzati - Nata.
							
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved