Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Nashon William Bidyanguze
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigoma Kusini
Primary Question
MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji katika Mbuga ya Kalola, Kijiji cha Nguruka – Uvinza?
Supplementary Question 1
MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ni hizi Skimu za Kashagulu, Mgambazi, Nkonkwa na Ilagala, baadhi yake ziliwahi kuwa zinafanya kazi; na kwa kuwa tegemeo la wananchi ni kwenye kilimo cha umwagiliaji, je, ni lini sasa upembuzi yakinifu huu wa ukarabati utakamilika?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kwenye Skimu hii ya Kalola; hili ni bonde kubwa sana kama Serikali inavyotambua kwamba ni hekta 20,000. Hii skimu ikienda kujengwa itahudumia na kufaidisha wananchi takribani 100,000. Je, ni lini hii skimu pia itakwenda kukamilika upembuzi yakinifu wake? Ahsante. (Makofi)
 
											Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
								NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, tayari shughuli ya upembuzi yakinifu na upembuzi wa kina zinaendelea katika maeneo yote haya niliyoyataja ikiwemo hii skimu ya Kalola. Serikali inajua kabisa na kutambua umuhimu wa skimu hizi kwa ajili ya kuwasaidia wananchi. 
Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kweli kwa kufuatilia jambo hili, na nikuhakikishie katika mwaka ujao wa fedha 2025/2026 tayari mmeshatupitishia bajeti ya kwenda kutekeleza jukumu hili, ninawaomba wananchi wa maeneo haya yote wawe watulivu wakati Serikali inaendelea kutekeleza ukamilishaji wa skimu hizi.
							
 
											Name
Pauline Philipo Gekul
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Babati Mjini
Primary Question
MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji katika Mbuga ya Kalola, Kijiji cha Nguruka – Uvinza?
Supplementary Question 2
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante nikushukuru kwa nafasi. Skimu ya Umwagiliaji katika mtaa wa Gendi Kuu, Kata ya Singe, Jimbo la Babati Mjini ulitakiwa kuanza baada ya mvua kukatika na mvua zimeshakatika, hazinyeshi tena. Ni lini skimu hii itaanza, kwani wananchi wanasubiri?
 
											Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tumpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji. Kama alivyojieleza yeye mwenyewe, ni kweli kabisa mvua zimepungua. Ninaelekeza watalaam wetu waende site kule kuangalia uwezekano wa kuanza kwa skimu hii, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved